Swahili - Surah Al-Fajr ( The Dawn ) | المكتبة الإسلامية صدقة جارية عن المغفور لهم بإذن الله أحمد سليمان البراك وزوجته وابنائه سليمان ومحمد ويونس وابنته إيمان

,,

اللهم اجعل هذا العمل نافعاً لصاحبه يوم القيامة

ولمن ساهم وساعد بنشره

,,

Surah Al-Fajr ( The Dawn )

Swahili

Surah Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya count 30
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email
وَالْفَجْرِ ( 1 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 1
Naapa kwa alfajiri,
وَلَيَالٍ عَشْرٍ ( 2 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 2
Na kwa masiku kumi,
وَالشَّفْعِ وَالْوَتْرِ ( 3 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 3
Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,
وَاللَّيْلِ إِذَا يَسْرِ ( 4 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 4
Na kwa usiku unapo pita,
هَلْ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٌ لِّذِي حِجْرٍ ( 5 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 5
Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?
أَلَمْ تَرَ كَيْفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ ( 6 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 6
Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?
إِرَمَ ذَاتِ الْعِمَادِ ( 7 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 7
Wa Iram, wenye majumba marefu?
الَّتِي لَمْ يُخْلَقْ مِثْلُهَا فِي الْبِلَادِ ( 8 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 8
Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?
وَثَمُودَ الَّذِينَ جَابُوا الصَّخْرَ بِالْوَادِ ( 9 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 9
Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?
وَفِرْعَوْنَ ذِي الْأَوْتَادِ ( 10 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 10
Na Firauni mwenye vigingi?
الَّذِينَ طَغَوْا فِي الْبِلَادِ ( 11 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 11
Ambao walifanya jeuri katika nchi?
فَأَكْثَرُوا فِيهَا الْفَسَادَ ( 12 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 12
Wakakithirisha humo ufisadi?
فَصَبَّ عَلَيْهِمْ رَبُّكَ سَوْطَ عَذَابٍ ( 13 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 13
Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.
إِنَّ رَبَّكَ لَبِالْمِرْصَادِ ( 14 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 14
Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.
فَأَمَّا الْإِنسَانُ إِذَا مَا ابْتَلَاهُ رَبُّهُ فَأَكْرَمَهُ وَنَعَّمَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَكْرَمَنِ ( 15 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 15
Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!
وَأَمَّا إِذَا مَا ابْتَلَاهُ فَقَدَرَ عَلَيْهِ رِزْقَهُ فَيَقُولُ رَبِّي أَهَانَنِ ( 16 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 16
Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!
كَلَّا ۖ بَل لَّا تُكْرِمُونَ الْيَتِيمَ ( 17 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 17
Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,
وَلَا تَحَاضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ الْمِسْكِينِ ( 18 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 18
Wala hamhimizani kulisha masikini;
وَتَأْكُلُونَ التُّرَاثَ أَكْلًا لَّمًّا ( 19 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 19
Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,
وَتُحِبُّونَ الْمَالَ حُبًّا جَمًّا ( 20 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 20
Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.
كَلَّا إِذَا دُكَّتِ الْأَرْضُ دَكًّا دَكًّا ( 21 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 21
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
وَجَاءَ رَبُّكَ وَالْمَلَكُ صَفًّا صَفًّا ( 22 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 22
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
وَجِيءَ يَوْمَئِذٍ بِجَهَنَّمَ ۚ يَوْمَئِذٍ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ وَأَنَّىٰ لَهُ الذِّكْرَىٰ ( 23 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 23
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
يَقُولُ يَا لَيْتَنِي قَدَّمْتُ لِحَيَاتِي ( 24 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 24
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!
فَيَوْمَئِذٍ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُ أَحَدٌ ( 25 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 25
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُ أَحَدٌ ( 26 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 26
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.
يَا أَيَّتُهَا النَّفْسُ الْمُطْمَئِنَّةُ ( 27 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 27
Ewe nafsi iliyo tua!
ارْجِعِي إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةً مَّرْضِيَّةً ( 28 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 28
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.
فَادْخُلِي فِي عِبَادِي ( 29 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 29
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
وَادْخُلِي جَنَّتِي ( 30 ) Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya 30
Na ingia katika Pepo yangu.
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email

Select language

Select surah