Swahili - Surah As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) | المكتبة الإسلامية صدقة جارية عن المغفور لهم بإذن الله أحمد سليمان البراك وزوجته وابنائه سليمان ومحمد ويونس وابنته إيمان

,,

اللهم اجعل هذا العمل نافعاً لصاحبه يوم القيامة

ولمن ساهم وساعد بنشره

,,

Surah As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks )

Swahili

Surah As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya count 182
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email
وَالصَّافَّاتِ صَفًّا ( 1 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 1
Naapa kwa wanao jipanga kwa safu.
فَالزَّاجِرَاتِ زَجْرًا ( 2 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 2
Na kwa wenye kukataza mabaya.
فَالتَّالِيَاتِ ذِكْرًا ( 3 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 3
Na kwa wenye kusoma Ukumbusho.
إِنَّ إِلَٰهَكُمْ لَوَاحِدٌ ( 4 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 4
Hakika Mungu wenu bila ya shaka ni Mmoja.
رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا وَرَبُّ الْمَشَارِقِ ( 5 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 5
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na yaliyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote.
إِنَّا زَيَّنَّا السَّمَاءَ الدُّنْيَا بِزِينَةٍ الْكَوَاكِبِ ( 6 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 6
Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota.
وَحِفْظًا مِّن كُلِّ شَيْطَانٍ مَّارِدٍ ( 7 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 7
Na kulinda na kila shet'ani a'si.
لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى الْمَلَإِ الْأَعْلَىٰ وَيُقْذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٍ ( 8 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 8
Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande.
دُحُورًا ۖ وَلَهُمْ عَذَابٌ وَاصِبٌ ( 9 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 9
Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu.
إِلَّا مَنْ خَطِفَ الْخَطْفَةَ فَأَتْبَعَهُ شِهَابٌ ثَاقِبٌ ( 10 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 10
Isipo kuwa anaye nyakua kitu kidogo, na mara humfwatia kimondo kinacho ng'ara.
فَاسْتَفْتِهِمْ أَهُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَم مَّنْ خَلَقْنَا ۚ إِنَّا خَلَقْنَاهُم مِّن طِينٍ لَّازِبٍ ( 11 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 11
Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba. Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata.
بَلْ عَجِبْتَ وَيَسْخَرُونَ ( 12 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 12
Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara.
وَإِذَا ذُكِّرُوا لَا يَذْكُرُونَ ( 13 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 13
Na wanapo kumbushwa hawakumbuki.
وَإِذَا رَأَوْا آيَةً يَسْتَسْخِرُونَ ( 14 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 14
Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara.
وَقَالُوا إِنْ هَٰذَا إِلَّا سِحْرٌ مُّبِينٌ ( 15 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 15
Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri.
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ ( 16 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 16
Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?
أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ ( 17 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 17
Hata baba zetu wa zamani?
قُلْ نَعَمْ وَأَنتُمْ دَاخِرُونَ ( 18 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 18
Sema: Naam! Hali nanyi ni madhalili.
فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ فَإِذَا هُمْ يَنظُرُونَ ( 19 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 19
Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!
وَقَالُوا يَا وَيْلَنَا هَٰذَا يَوْمُ الدِّينِ ( 20 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 20
Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo.
هَٰذَا يَوْمُ الْفَصْلِ الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ ( 21 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 21
Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyo kuwa mkiikadhibisha.
احْشُرُوا الَّذِينَ ظَلَمُوا وَأَزْوَاجَهُمْ وَمَا كَانُوا يَعْبُدُونَ ( 22 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 22
Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu -
مِن دُونِ اللَّهِ فَاهْدُوهُمْ إِلَىٰ صِرَاطِ الْجَحِيمِ ( 23 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 23
Badala ya Mwenyezi Mungu. Waongozeni njia ya Jahannamu!
وَقِفُوهُمْ ۖ إِنَّهُم مَّسْئُولُونَ ( 24 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 24
Na wasimamisheni. Hakika hao watasailiwa:
مَا لَكُمْ لَا تَنَاصَرُونَ ( 25 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 25
Mna nini? Mbona hamsaidiani?
بَلْ هُمُ الْيَوْمَ مُسْتَسْلِمُونَ ( 26 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 26
Bali hii leo, watasalimu amri.
وَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ ( 27 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 27
Watakabiliana wao kwa wao kuulizana.
قَالُوا إِنَّكُمْ كُنتُمْ تَأْتُونَنَا عَنِ الْيَمِينِ ( 28 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 28
Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia.
قَالُوا بَل لَّمْ تَكُونُوا مُؤْمِنِينَ ( 29 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 29
Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini.
وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيْكُم مِّن سُلْطَانٍ ۖ بَلْ كُنتُمْ قَوْمًا طَاغِينَ ( 30 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 30
Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu.
فَحَقَّ عَلَيْنَا قَوْلُ رَبِّنَا ۖ إِنَّا لَذَائِقُونَ ( 31 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 31
Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu.
فَأَغْوَيْنَاكُمْ إِنَّا كُنَّا غَاوِينَ ( 32 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 32
Tulikupotezeni kwa sababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu.
فَإِنَّهُمْ يَوْمَئِذٍ فِي الْعَذَابِ مُشْتَرِكُونَ ( 33 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 33
Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفْعَلُ بِالْمُجْرِمِينَ ( 34 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 34
Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu.
إِنَّهُمْ كَانُوا إِذَا قِيلَ لَهُمْ لَا إِلَٰهَ إِلَّا اللَّهُ يَسْتَكْبِرُونَ ( 35 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 35
Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa 'Llahu Hapana mungu ila Mwenyezi Mungu tu, wakijivuna.
وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُو آلِهَتِنَا لِشَاعِرٍ مَّجْنُونٍ ( 36 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 36
Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?
بَلْ جَاءَ بِالْحَقِّ وَصَدَّقَ الْمُرْسَلِينَ ( 37 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 37
Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume.
إِنَّكُمْ لَذَائِقُو الْعَذَابِ الْأَلِيمِ ( 38 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 38
Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu.
وَمَا تُجْزَوْنَ إِلَّا مَا كُنتُمْ تَعْمَلُونَ ( 39 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 39
Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya.
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ( 40 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 40
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
أُولَٰئِكَ لَهُمْ رِزْقٌ مَّعْلُومٌ ( 41 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 41
Hao ndio watakao pata riziki maalumu,
فَوَاكِهُ ۖ وَهُم مُّكْرَمُونَ ( 42 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 42
Matunda, nao watahishimiwa.
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ ( 43 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 43
Katika Bustani za neema.
عَلَىٰ سُرُرٍ مُّتَقَابِلِينَ ( 44 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 44
Wako juu ya viti wamekabiliana.
يُطَافُ عَلَيْهِم بِكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ ( 45 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 45
Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem
بَيْضَاءَ لَذَّةٍ لِّلشَّارِبِينَ ( 46 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 46
Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao.
لَا فِيهَا غَوْلٌ وَلَا هُمْ عَنْهَا يُنزَفُونَ ( 47 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 47
Hakina madhara, wala hakiwaleweshi.
وَعِندَهُمْ قَاصِرَاتُ الطَّرْفِ عِينٌ ( 48 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 48
Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri.
كَأَنَّهُنَّ بَيْضٌ مَّكْنُونٌ ( 49 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 49
Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika.
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَسَاءَلُونَ ( 50 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 50
Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe.
قَالَ قَائِلٌ مِّنْهُمْ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٌ ( 51 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 51
Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki
يَقُولُ أَإِنَّكَ لَمِنَ الْمُصَدِّقِينَ ( 52 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 52
Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki
أَإِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَدِينُونَ ( 53 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 53
Ati tukisha kufa tukawa udongo na mafupa, ndio tutalipwa na kuhisabiwa?
قَالَ هَلْ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ ( 54 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 54
Atasema: Je! Nyie mnawaona?
فَاطَّلَعَ فَرَآهُ فِي سَوَاءِ الْجَحِيمِ ( 55 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 55
Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu.
قَالَ تَاللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرْدِينِ ( 56 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 56
Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza.
وَلَوْلَا نِعْمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ الْمُحْضَرِينَ ( 57 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 57
Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningeli kuwa miongoni mwa walio hudhurishwa.
أَفَمَا نَحْنُ بِمَيِّتِينَ ( 58 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 58
Je! Sisi hatutakufa,
إِلَّا مَوْتَتَنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ ( 59 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 59
Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa.
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ ( 60 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 60
Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa.
لِمِثْلِ هَٰذَا فَلْيَعْمَلِ الْعَامِلُونَ ( 61 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 61
Kwa mfano wa haya nawatende watendao.
أَذَٰلِكَ خَيْرٌ نُّزُلًا أَمْ شَجَرَةُ الزَّقُّومِ ( 62 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 62
Je! Kukaribishwa hivi si ndio bora, au mti wa Zaqqum?
إِنَّا جَعَلْنَاهَا فِتْنَةً لِّلظَّالِمِينَ ( 63 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 63
Hakika Sisi tumeufanya huo kuwa ni mateso kwa walio dhulumu.
إِنَّهَا شَجَرَةٌ تَخْرُجُ فِي أَصْلِ الْجَحِيمِ ( 64 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 64
Hakika huo ni mti unao toka katikati ya Jahannamu.
طَلْعُهَا كَأَنَّهُ رُءُوسُ الشَّيَاطِينِ ( 65 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 65
Mashada ya matunda yake kama kwamba vichwa vya mashet'ani.
فَإِنَّهُمْ لَآكِلُونَ مِنْهَا فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ ( 66 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 66
Basi hakika bila ya shaka hao watayala hayo, na wajaze matumbo.
ثُمَّ إِنَّ لَهُمْ عَلَيْهَا لَشَوْبًا مِّنْ حَمِيمٍ ( 67 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 67
Kisha juu yake wanyweshwe mchanganyo wa maji yamoto yaliyo chemka.
ثُمَّ إِنَّ مَرْجِعَهُمْ لَإِلَى الْجَحِيمِ ( 68 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 68
Kisha hakika marejeo yao bila ya shaka yatakuwa kwenye Jahannamu.
إِنَّهُمْ أَلْفَوْا آبَاءَهُمْ ضَالِّينَ ( 69 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 69
Hakika waliwakuta baba zao wamepotea.
فَهُمْ عَلَىٰ آثَارِهِمْ يُهْرَعُونَ ( 70 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 70
Na wao wakafanya haraka kufuata nyayo zao.
وَلَقَدْ ضَلَّ قَبْلَهُمْ أَكْثَرُ الْأَوَّلِينَ ( 71 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 71
Na bila ya shaka walikwisha potea kabla yao wengi wa watu wa zamani.
وَلَقَدْ أَرْسَلْنَا فِيهِم مُّنذِرِينَ ( 72 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 72
Na Sisi hakika tuliwapelekea waonyaji.
فَانظُرْ كَيْفَ كَانَ عَاقِبَةُ الْمُنذَرِينَ ( 73 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 73
Basi hebu angalia ulikuwaje mwisho wa walio onywa.
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ( 74 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 74
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio khitariwa.
وَلَقَدْ نَادَانَا نُوحٌ فَلَنِعْمَ الْمُجِيبُونَ ( 75 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 75
Na hakika Nuhu alitwita, na Sisi ni bora wa waitikiaji.
وَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ ( 76 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 76
Na tulimwokoa yeye na ahali zake kutokana na msiba mkubwa.
وَجَعَلْنَا ذُرِّيَّتَهُ هُمُ الْبَاقِينَ ( 77 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 77
Na tuliwajaalia dhuriya zake ndio wenye kubakia.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ ( 78 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 78
Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye.
سَلَامٌ عَلَىٰ نُوحٍ فِي الْعَالَمِينَ ( 79 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 79
Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ( 80 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 80
Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ( 81 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 81
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
ثُمَّ أَغْرَقْنَا الْآخَرِينَ ( 82 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 82
Kisha tukawazamisha wale wengine.
وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِ لَإِبْرَاهِيمَ ( 83 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 83
Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,
إِذْ جَاءَ رَبَّهُ بِقَلْبٍ سَلِيمٍ ( 84 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 84
Alipo mjia Mola wake Mlezi kwa moyo mzima.
إِذْ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوْمِهِ مَاذَا تَعْبُدُونَ ( 85 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 85
Alimwambia baba yake na watu wake: Mnaabudu nini?
أَئِفْكًا آلِهَةً دُونَ اللَّهِ تُرِيدُونَ ( 86 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 86
Kwa kuzua tu mnataka miungu mingine badala ya Mwenyezi Mungu?
فَمَا ظَنُّكُم بِرَبِّ الْعَالَمِينَ ( 87 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 87
Mnamdhania nini Mola Mlezi wa walimwengu wote?
فَنَظَرَ نَظْرَةً فِي النُّجُومِ ( 88 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 88
Kisha akapiga jicho kutazama nyota.
فَقَالَ إِنِّي سَقِيمٌ ( 89 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 89
Akasema: Hakika mimi ni mgonjwa!
فَتَوَلَّوْا عَنْهُ مُدْبِرِينَ ( 90 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 90
Nao wakamwacha, wakampa kisogo.
فَرَاغَ إِلَىٰ آلِهَتِهِمْ فَقَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ ( 91 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 91
Basi akaiendea miungu yao kwa siri, akaiambia: Mbona hamli?
مَا لَكُمْ لَا تَنطِقُونَ ( 92 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 92
Mna nini hata hamsemi?
فَرَاغَ عَلَيْهِمْ ضَرْبًا بِالْيَمِينِ ( 93 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 93
Kisha akaigeukia kuipiga kwa mkono wa kulia.
فَأَقْبَلُوا إِلَيْهِ يَزِفُّونَ ( 94 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 94
Basi wakamjia upesi upesi.
قَالَ أَتَعْبُدُونَ مَا تَنْحِتُونَ ( 95 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 95
Akasema: Hivyo mnaviabudu vitu mnavyo vichonga wenyewe?
وَاللَّهُ خَلَقَكُمْ وَمَا تَعْمَلُونَ ( 96 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 96
Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mnavyo vifanya!
قَالُوا ابْنُوا لَهُ بُنْيَانًا فَأَلْقُوهُ فِي الْجَحِيمِ ( 97 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 97
Wakasema: Mjengeeni jengo, na kisha mtupeni motoni humo!
فَأَرَادُوا بِهِ كَيْدًا فَجَعَلْنَاهُمُ الْأَسْفَلِينَ ( 98 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 98
Basi walitaka kumfanyia vitimbi, lakini tukawafanya wao ndio wa chini.
وَقَالَ إِنِّي ذَاهِبٌ إِلَىٰ رَبِّي سَيَهْدِينِ ( 99 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 99
Na akasema: Hakika mimi nahama, nakwenda kwa Mola wangu Mlezi; Yeye ataniongoa.
رَبِّ هَبْ لِي مِنَ الصَّالِحِينَ ( 100 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 100
Ewe Mola wangu Mlezi! Nitunukie aliye miongoni mwa watenda mema.
فَبَشَّرْنَاهُ بِغُلَامٍ حَلِيمٍ ( 101 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 101
Basi tukambashiria mwana aliye mpole.
فَلَمَّا بَلَغَ مَعَهُ السَّعْيَ قَالَ يَا بُنَيَّ إِنِّي أَرَىٰ فِي الْمَنَامِ أَنِّي أَذْبَحُكَ فَانظُرْ مَاذَا تَرَىٰ ۚ قَالَ يَا أَبَتِ افْعَلْ مَا تُؤْمَرُ ۖ سَتَجِدُنِي إِن شَاءَ اللَّهُ مِنَ الصَّابِرِينَ ( 102 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 102
Basi alipo fika makamo ya kwenda na kurudi pamoja naye, alimwambia: Ewe mwanangu! Hakika mimi nimeona usingizini kuwa ninakuchinja. Basi angalia wewe, waonaje? Akasema: Ewe baba yangu! Tenda unavyo amrishwa, utanikuta mimi, Inshallah, katika wanao subiri.
فَلَمَّا أَسْلَمَا وَتَلَّهُ لِلْجَبِينِ ( 103 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 103
Basi wote wawili walipo jisalimisha, na akamlaza juu ya kipaji.
وَنَادَيْنَاهُ أَن يَا إِبْرَاهِيمُ ( 104 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 104
Tulimwita: Ewe Ibrahim!
قَدْ صَدَّقْتَ الرُّؤْيَا ۚ إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ( 105 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 105
Umekwisha itimiliza ndoto. Hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao tenda mema.
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ الْبَلَاءُ الْمُبِينُ ( 106 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 106
Hakika haya ni majaribio yaliyo dhaahiri.
وَفَدَيْنَاهُ بِذِبْحٍ عَظِيمٍ ( 107 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 107
Basi tukamtolea fidia kwa dhabihu mtukufu.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ ( 108 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 108
Na tukamwachia (sifa njema) kwa watu walio kuja baadaye.
سَلَامٌ عَلَىٰ إِبْرَاهِيمَ ( 109 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 109
Iwe salama kwa Ibrahim!
كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ( 110 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 110
Hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema.
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ( 111 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 111
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
وَبَشَّرْنَاهُ بِإِسْحَاقَ نَبِيًّا مِّنَ الصَّالِحِينَ ( 112 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 112
Na tukambashiria kuzaliwa Is-haqa, naye ni Nabii miongoni mwa watu wema.
وَبَارَكْنَا عَلَيْهِ وَعَلَىٰ إِسْحَاقَ ۚ وَمِن ذُرِّيَّتِهِمَا مُحْسِنٌ وَظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ مُبِينٌ ( 113 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 113
Na tukambarikia yeye na Is-haqa. Na miongoni mwa dhuriya zao walitokea wema na wenye kudhulumu nafsi zao waziwazi.
وَلَقَدْ مَنَنَّا عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ ( 114 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 114
Na kwa hakika tuliwafanyia hisani Musa na Haruni.
وَنَجَّيْنَاهُمَا وَقَوْمَهُمَا مِنَ الْكَرْبِ الْعَظِيمِ ( 115 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 115
Na tukawaokoa wao na watu wao kutokana na dhiki kubwa.
وَنَصَرْنَاهُمْ فَكَانُوا هُمُ الْغَالِبِينَ ( 116 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 116
Na tukawanusuru; na wakawa wao ndio wenye kushinda.
وَآتَيْنَاهُمَا الْكِتَابَ الْمُسْتَبِينَ ( 117 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 117
Na tukawapa wawili hao Kitabu kinacho bainisha.
وَهَدَيْنَاهُمَا الصِّرَاطَ الْمُسْتَقِيمَ ( 118 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 118
Na tukawaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِمَا فِي الْآخِرِينَ ( 119 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 119
Na tukawaachia (sifa njema) katika watu walio kuja baadaye.
سَلَامٌ عَلَىٰ مُوسَىٰ وَهَارُونَ ( 120 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 120
Iwe salama kwa Musa na Haruni!
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ( 121 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 121
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
إِنَّهُمَا مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ( 122 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 122
Hakika wawili hao ni katika waja wetu walio amini.
وَإِنَّ إِلْيَاسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ ( 123 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 123
Na hakika Ilyas bila ya shaka alikuwa miongoni mwa Mitume.
إِذْ قَالَ لِقَوْمِهِ أَلَا تَتَّقُونَ ( 124 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 124
Alipo waambia watu wake: Hamwogopi?
أَتَدْعُونَ بَعْلًا وَتَذَرُونَ أَحْسَنَ الْخَالِقِينَ ( 125 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 125
Mnamwomba Baa'li na mnamwacha Mbora wa waumbaji,
اللَّهَ رَبَّكُمْ وَرَبَّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ ( 126 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 126
Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?
فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ ( 127 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 127
Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ( 128 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 128
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
وَتَرَكْنَا عَلَيْهِ فِي الْآخِرِينَ ( 129 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 129
Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye.
سَلَامٌ عَلَىٰ إِلْ يَاسِينَ ( 130 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 130
Iwe salama kwa Ilyas.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجْزِي الْمُحْسِنِينَ ( 131 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 131
Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema.
إِنَّهُ مِنْ عِبَادِنَا الْمُؤْمِنِينَ ( 132 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 132
Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini.
وَإِنَّ لُوطًا لَّمِنَ الْمُرْسَلِينَ ( 133 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 133
Na hakika Lut'i bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume.
إِذْ نَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ أَجْمَعِينَ ( 134 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 134
Tulipo mwokoa yeye na ahali zake wote,
إِلَّا عَجُوزًا فِي الْغَابِرِينَ ( 135 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 135
Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma.
ثُمَّ دَمَّرْنَا الْآخَرِينَ ( 136 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 136
Kisha tukawaangamiza wale wengineo.
وَإِنَّكُمْ لَتَمُرُّونَ عَلَيْهِم مُّصْبِحِينَ ( 137 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 137
Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,
وَبِاللَّيْلِ ۗ أَفَلَا تَعْقِلُونَ ( 138 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 138
Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?
وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ الْمُرْسَلِينَ ( 139 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 139
Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume.
إِذْ أَبَقَ إِلَى الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ ( 140 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 140
Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni.
فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ الْمُدْحَضِينَ ( 141 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 141
Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa.
فَالْتَقَمَهُ الْحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٌ ( 142 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 142
Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa.
فَلَوْلَا أَنَّهُ كَانَ مِنَ الْمُسَبِّحِينَ ( 143 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 143
Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Mwenyezi Mungu,
لَلَبِثَ فِي بَطْنِهِ إِلَىٰ يَوْمِ يُبْعَثُونَ ( 144 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 144
Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa.
فَنَبَذْنَاهُ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ سَقِيمٌ ( 145 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 145
Lakini tulimtupa ufukweni patupu, hali yu mgonjwa.
وَأَنبَتْنَا عَلَيْهِ شَجَرَةً مِّن يَقْطِينٍ ( 146 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 146
Na tukauotesha juu yake mmea wa kabila ya mung'unye.
وَأَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ مِائَةِ أَلْفٍ أَوْ يَزِيدُونَ ( 147 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 147
Na tulimtuma kwa watu laki moja au zaidi.
فَآمَنُوا فَمَتَّعْنَاهُمْ إِلَىٰ حِينٍ ( 148 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 148
Basi wakaamini, na tukawastarehesha kwa muda.
فَاسْتَفْتِهِمْ أَلِرَبِّكَ الْبَنَاتُ وَلَهُمُ الْبَنُونَ ( 149 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 149
Basi waulize: Ati Mola wako Mlezi ndiye mwenye watoto wa kike, na wao wanao watoto wa kiume?
أَمْ خَلَقْنَا الْمَلَائِكَةَ إِنَاثًا وَهُمْ شَاهِدُونَ ( 150 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 150
Au tumewaumba Malaika kuwa ni wanawake, na wao wakashuhudia?
أَلَا إِنَّهُم مِّنْ إِفْكِهِمْ لَيَقُولُونَ ( 151 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 151
Ati ni kwa uzushi wao ndio wanasema:
وَلَدَ اللَّهُ وَإِنَّهُمْ لَكَاذِبُونَ ( 152 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 152
Mwenyezi Mungu amezaa! Ama hakika bila ya shaka hao ni waongo!
أَصْطَفَى الْبَنَاتِ عَلَى الْبَنِينَ ( 153 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 153
Ati amekhiari watoto wa kike kuliko wanaume?
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ ( 154 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 154
Mna nini? Mnahukumu vipi nyinyi?
أَفَلَا تَذَكَّرُونَ ( 155 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 155
Hamkumbuki?
أَمْ لَكُمْ سُلْطَانٌ مُّبِينٌ ( 156 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 156
Au mnayo hoja iliyo wazi?
فَأْتُوا بِكِتَابِكُمْ إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ( 157 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 157
Basi leteni Kitabu chenu kama mnasema kweli.
وَجَعَلُوا بَيْنَهُ وَبَيْنَ الْجِنَّةِ نَسَبًا ۚ وَلَقَدْ عَلِمَتِ الْجِنَّةُ إِنَّهُمْ لَمُحْضَرُونَ ( 158 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 158
Na wameweka makhusiano ya nasaba baina yake na majini; na majini wamekwisha jua bila ya shaka kuwa wao watahudhurishwa.
سُبْحَانَ اللَّهِ عَمَّا يَصِفُونَ ( 159 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 159
Subhana 'Llah Ametakasika Mwenyezi Mungu na hayo wanayo msingizia.
إِلَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ( 160 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 160
Isipo kuwa waja wa Mwenyezi Mungu walio safishwa.
فَإِنَّكُمْ وَمَا تَعْبُدُونَ ( 161 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 161
Basi hakika nyinyi na mnao waabudu
مَا أَنتُمْ عَلَيْهِ بِفَاتِنِينَ ( 162 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 162
Hamwezi kuwapoteza
إِلَّا مَنْ هُوَ صَالِ الْجَحِيمِ ( 163 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 163
Isipo kuwa yule atakaye ingia Motoni.
وَمَا مِنَّا إِلَّا لَهُ مَقَامٌ مَّعْلُومٌ ( 164 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 164
Na hapana katika sisi ila anapo mahali pake maalumu.
وَإِنَّا لَنَحْنُ الصَّافُّونَ ( 165 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 165
Na hakika bila ya shaka sisi ndio wajipangao safu.
وَإِنَّا لَنَحْنُ الْمُسَبِّحُونَ ( 166 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 166
Na hakika sisi ndio wenye kusabihi kutakasa.
وَإِن كَانُوا لَيَقُولُونَ ( 167 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 167
Na walikuwapo walio kuwa wakisema:
لَوْ أَنَّ عِندَنَا ذِكْرًا مِّنَ الْأَوَّلِينَ ( 168 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 168
Tungeli kuwa na Ukumbusho kama wa watu wa zamani,
لَكُنَّا عِبَادَ اللَّهِ الْمُخْلَصِينَ ( 169 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 169
Bila ya shaka tungeli kuwa ni waja wa Mwenyezi Mungu wenye ikhlasi.
فَكَفَرُوا بِهِ ۖ فَسَوْفَ يَعْلَمُونَ ( 170 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 170
Lakini waliukataa. Basi watakuja jua.
وَلَقَدْ سَبَقَتْ كَلِمَتُنَا لِعِبَادِنَا الْمُرْسَلِينَ ( 171 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 171
Na bila ya shaka neno letu lilikwisha tangulia kwa waja wetu walio tumwa.
إِنَّهُمْ لَهُمُ الْمَنصُورُونَ ( 172 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 172
Ya kuwa wao bila ya shaka ndio watakao nusuriwa.
وَإِنَّ جُندَنَا لَهُمُ الْغَالِبُونَ ( 173 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 173
Na kwamba jeshi letu ndilo litakalo shinda.
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ ( 174 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 174
Basi waachilie mbali kwa muda.
وَأَبْصِرْهُمْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ ( 175 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 175
Na watazame, nao wataona.
أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ ( 176 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 176
Je! Wanaihimiza adhabu yetu?
فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمْ فَسَاءَ صَبَاحُ الْمُنذَرِينَ ( 177 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 177
Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa.
وَتَوَلَّ عَنْهُمْ حَتَّىٰ حِينٍ ( 178 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 178
Na waache kwa muda.
وَأَبْصِرْ فَسَوْفَ يُبْصِرُونَ ( 179 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 179
Na tazama, na wao wataona.
سُبْحَانَ رَبِّكَ رَبِّ الْعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ ( 180 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 180
Subhana Rabbi'l'Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia.
وَسَلَامٌ عَلَى الْمُرْسَلِينَ ( 181 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 181
Na Salamu juu ya Mitume.
وَالْحَمْدُ لِلَّهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ( 182 ) As-Saaffat ( Those Ranges in Ranks ) - Aya 182
Na sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email

Select language

Select surah