Swahili - Surah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) | المكتبة الإسلامية صدقة جارية عن المغفور لهم بإذن الله أحمد سليمان البراك وزوجته وابنائه سليمان ومحمد ويونس وابنته إيمان

,,

اللهم اجعل هذا العمل نافعاً لصاحبه يوم القيامة

ولمن ساهم وساعد بنشره

,,

Surah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud)

Swahili

Surah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya count 36
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email
وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ( 1 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 1
Ole wao hao wapunjao!
الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ ( 2 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 2
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ ( 3 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 3
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
أَلَا يَظُنُّ أُولَٰئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ ( 4 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 4
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
لِيَوْمٍ عَظِيمٍ ( 5 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 5
Katika Siku iliyo kuu,
يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ ( 6 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 6
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٍ ( 7 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 7
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا سِجِّينٌ ( 8 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 8
Unajua nini Sijjin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌ ( 9 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 9
Kitabu kilicho andikwa.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ ( 10 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 10
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
الَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ ( 11 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 11
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
وَمَا يُكَذِّبُ بِهِ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ ( 12 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 12
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ ( 13 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 13
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا يَكْسِبُونَ ( 14 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 14
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
كَلَّا إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّمَحْجُوبُونَ ( 15 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 15
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُو الْجَحِيمِ ( 16 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 16
Kisha wataingia Motoni!
ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ ( 17 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 17
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْأَبْرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ ( 18 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 18
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا عِلِّيُّونَ ( 19 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 19
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌ ( 20 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 20
Kitabu kilicho andikwa.
يَشْهَدُهُ الْمُقَرَّبُونَ ( 21 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 21
Wanakishuhudia walio karibishwa.
إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ ( 22 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 22
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ ( 23 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 23
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
تَعْرِفُ فِي وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ النَّعِيمِ ( 24 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 24
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍ مَّخْتُومٍ ( 25 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 25
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
خِتَامُهُ مِسْكٌ ۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ ( 26 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 26
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
وَمِزَاجُهُ مِن تَسْنِيمٍ ( 27 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 27
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا الْمُقَرَّبُونَ ( 28 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 28
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُوا مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَ ( 29 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 29
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
وَإِذَا مَرُّوا بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ ( 30 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 30
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
وَإِذَا انقَلَبُوا إِلَىٰ أَهْلِهِمُ انقَلَبُوا فَكِهِينَ ( 31 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 31
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوا إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَضَالُّونَ ( 32 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 32
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
وَمَا أُرْسِلُوا عَلَيْهِمْ حَافِظِينَ ( 33 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 33
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ ( 34 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 34
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ ( 35 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 35
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
هَلْ ثُوِّبَ الْكُفَّارُ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ ( 36 ) Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya 36
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email

Select language

Select surah