Swahili - Surah Ad-Dukhan ( The Smoke ) | المكتبة الإسلامية صدقة جارية عن المغفور لهم بإذن الله أحمد سليمان البراك وزوجته وابنائه سليمان ومحمد ويونس وابنته إيمان

,,

اللهم اجعل هذا العمل نافعاً لصاحبه يوم القيامة

ولمن ساهم وساعد بنشره

,,

Surah Ad-Dukhan ( The Smoke )

Swahili

Surah Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya count 59
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email
حم ( 1 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 1
H'a Mim
وَالْكِتَابِ الْمُبِينِ ( 2 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 2
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ ۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ ( 3 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 3
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ ( 4 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 4
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
أَمْرًا مِّنْ عِندِنَا ۚ إِنَّا كُنَّا مُرْسِلِينَ ( 5 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 5
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
رَحْمَةً مِّن رَّبِّكَ ۚ إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ( 6 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 6
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
رَبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ ( 7 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 7
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحْيِي وَيُمِيتُ ۖ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ ( 8 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 8
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
بَلْ هُمْ فِي شَكٍّ يَلْعَبُونَ ( 9 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 9
Lakini wao wanacheza katika shaka.
فَارْتَقِبْ يَوْمَ تَأْتِي السَّمَاءُ بِدُخَانٍ مُّبِينٍ ( 10 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 10
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
يَغْشَى النَّاسَ ۖ هَٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٌ ( 11 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 11
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
رَّبَّنَا اكْشِفْ عَنَّا الْعَذَابَ إِنَّا مُؤْمِنُونَ ( 12 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 12
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
أَنَّىٰ لَهُمُ الذِّكْرَىٰ وَقَدْ جَاءَهُمْ رَسُولٌ مُّبِينٌ ( 13 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 13
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
ثُمَّ تَوَلَّوْا عَنْهُ وَقَالُوا مُعَلَّمٌ مَّجْنُونٌ ( 14 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 14
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
إِنَّا كَاشِفُو الْعَذَابِ قَلِيلًا ۚ إِنَّكُمْ عَائِدُونَ ( 15 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 15
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
يَوْمَ نَبْطِشُ الْبَطْشَةَ الْكُبْرَىٰ إِنَّا مُنتَقِمُونَ ( 16 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 16
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
وَلَقَدْ فَتَنَّا قَبْلَهُمْ قَوْمَ فِرْعَوْنَ وَجَاءَهُمْ رَسُولٌ كَرِيمٌ ( 17 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 17
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
أَنْ أَدُّوا إِلَيَّ عِبَادَ اللَّهِ ۖ إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ( 18 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 18
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
وَأَن لَّا تَعْلُوا عَلَى اللَّهِ ۖ إِنِّي آتِيكُم بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ ( 19 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 19
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
وَإِنِّي عُذْتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمْ أَن تَرْجُمُونِ ( 20 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 20
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
وَإِن لَّمْ تُؤْمِنُوا لِي فَاعْتَزِلُونِ ( 21 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 21
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
فَدَعَا رَبَّهُ أَنَّ هَٰؤُلَاءِ قَوْمٌ مُّجْرِمُونَ ( 22 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 22
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
فَأَسْرِ بِعِبَادِي لَيْلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ ( 23 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 23
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
وَاتْرُكِ الْبَحْرَ رَهْوًا ۖ إِنَّهُمْ جُندٌ مُّغْرَقُونَ ( 24 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 24
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
كَمْ تَرَكُوا مِن جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ( 25 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 25
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
وَزُرُوعٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ ( 26 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 26
Na mimea na vyeo vitukufu!
وَنَعْمَةٍ كَانُوا فِيهَا فَاكِهِينَ ( 27 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 27
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
كَذَٰلِكَ ۖ وَأَوْرَثْنَاهَا قَوْمًا آخَرِينَ ( 28 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 28
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
فَمَا بَكَتْ عَلَيْهِمُ السَّمَاءُ وَالْأَرْضُ وَمَا كَانُوا مُنظَرِينَ ( 29 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 29
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
وَلَقَدْ نَجَّيْنَا بَنِي إِسْرَائِيلَ مِنَ الْعَذَابِ الْمُهِينِ ( 30 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 30
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
مِن فِرْعَوْنَ ۚ إِنَّهُ كَانَ عَالِيًا مِّنَ الْمُسْرِفِينَ ( 31 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 31
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
وَلَقَدِ اخْتَرْنَاهُمْ عَلَىٰ عِلْمٍ عَلَى الْعَالَمِينَ ( 32 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 32
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
وَآتَيْنَاهُم مِّنَ الْآيَاتِ مَا فِيهِ بَلَاءٌ مُّبِينٌ ( 33 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 33
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَيَقُولُونَ ( 34 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 34
Hakika hawa wanasema:
إِنْ هِيَ إِلَّا مَوْتَتُنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُنشَرِينَ ( 35 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 35
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
فَأْتُوا بِآبَائِنَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ( 36 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 36
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
أَهُمْ خَيْرٌ أَمْ قَوْمُ تُبَّعٍ وَالَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۚ أَهْلَكْنَاهُمْ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا مُجْرِمِينَ ( 37 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 37
Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا لَاعِبِينَ ( 38 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 38
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
مَا خَلَقْنَاهُمَا إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ( 39 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 39
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ مِيقَاتُهُمْ أَجْمَعِينَ ( 40 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 40
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
يَوْمَ لَا يُغْنِي مَوْلًى عَن مَّوْلًى شَيْئًا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ ( 41 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 41
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
إِلَّا مَن رَّحِمَ اللَّهُ ۚ إِنَّهُ هُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ( 42 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 42
Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
إِنَّ شَجَرَتَ الزَّقُّومِ ( 43 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 43
Hakika Mti wa Zaqqum,
طَعَامُ الْأَثِيمِ ( 44 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 44
Ni chakula cha mwenye dhambi.
كَالْمُهْلِ يَغْلِي فِي الْبُطُونِ ( 45 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 45
Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
كَغَلْيِ الْحَمِيمِ ( 46 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 46
Kama kutokota kwa maji ya moto.
خُذُوهُ فَاعْتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَاءِ الْجَحِيمِ ( 47 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 47
(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
ثُمَّ صُبُّوا فَوْقَ رَأْسِهِ مِنْ عَذَابِ الْحَمِيمِ ( 48 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 48
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
ذُقْ إِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْكَرِيمُ ( 49 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 49
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِ تَمْتَرُونَ ( 50 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 50
Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٍ ( 51 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 51
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ( 52 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 52
Katika mabustani na chemchem,
يَلْبَسُونَ مِن سُندُسٍ وَإِسْتَبْرَقٍ مُّتَقَابِلِينَ ( 53 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 53
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
كَذَٰلِكَ وَزَوَّجْنَاهُم بِحُورٍ عِينٍ ( 54 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 54
Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
يَدْعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَاكِهَةٍ آمِنِينَ ( 55 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 55
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
لَا يَذُوقُونَ فِيهَا الْمَوْتَ إِلَّا الْمَوْتَةَ الْأُولَىٰ ۖ وَوَقَاهُمْ عَذَابَ الْجَحِيمِ ( 56 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 56
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,
فَضْلًا مِّن رَّبِّكَ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ ( 57 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 57
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
فَإِنَّمَا يَسَّرْنَاهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ ( 58 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 58
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
فَارْتَقِبْ إِنَّهُم مُّرْتَقِبُونَ ( 59 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Aya 59
Ngoja tu, na wao wangoje pia.
Facebook Twitter Google+ Pinterest Reddit StumbleUpon Linkedin Tumblr Google Bookmarks Email

Select language

Select surah